23 Kisha akatengeneza Bahari* kwa madini yaliyoyeyushwa.+ Ilikuwa ya mviringo, yenye upana wa mikono 10 ukingo hadi ukingo na kimo cha mikono 5, na ingeweza kuzungukwa na kamba yenye urefu wa mikono 30.*+
25 Ilikuwa juu ya ng’ombe dume 12,+ watatu wakitazama kaskazini, watatu wakitazama magharibi, watatu wakitazama kusini, na watatu wakitazama mashariki; na Bahari hiyo ilikuwa juu yao, na sehemu zao zote za nyuma zilielekea katikati.