-
2 Wafalme 24:15, 16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Basi akampeleka Yehoyakini+ uhamishoni Babiloni;+ alimpeleka pia mama ya mfalme, wake za mfalme, maofisa wa makao yake, na viongozi wa nchi, akawapeleka uhamishoni Babiloni kutoka Yerusalemu. 16 Pia mfalme wa Babiloni aliwapeleka uhamishoni Babiloni mashujaa wote, 7,000, na vilevile mafundi na wahunzi* 1,000, wote walikuwa wanaume mashujaa waliozoezwa kupigana vita.
-
-
Yeremia 29:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
29 Haya ndiyo maneno ya barua ambayo nabii Yeremia aliwatumia kutoka Yerusalemu wazee waliobaki miongoni mwa watu waliopelekwa uhamishoni, makuhani, manabii, na watu wote, ambao Nebukadneza alikuwa amewatoa Yerusalemu na kuwapeleka uhamishoni Babiloni, 2 baada ya Mfalme Yekonia+ na mama malkia,+ maofisa wa makao ya mfalme, wakuu wa Yuda na Yerusalemu, na mafundi na wahunzi* kuondoka Yerusalemu.+
-