-
Kumbukumbu la Torati 30:8-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 “Kisha mtarudi na kuisikiliza sauti ya Yehova na kushika amri zake zote ninazowaamuru leo. 9 Yehova Mungu wenu atawaletea mafanikio mengi katika kazi yote ya mikono yenu,+ atawafanya muwe na watoto wengi na mifugo mingi na mazao mengi ya ardhi yenu, kwa maana Yehova atafurahia tena kuwafanikisha, kama alivyofurahia kuwafanikisha mababu zenu.+ 10 Kwa maana wakati huo mtaisikiliza sauti ya Yehova Mungu wenu na kushika amri zake na sheria zilizoandikwa katika kitabu hiki cha Sheria, nanyi mtarudi kwa Yehova Mungu wenu kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote.+
-