6 Yehova ana upanga; utafunikwa kwa damu.
Utafunikwa kwa mafuta,+
Kwa damu ya wanakondoo dume na mbuzi,
Kwa mafuta ya figo za kondoo dume.
Kwa maana Yehova ana dhabihu kule Bosra,
Machinjo makubwa katika nchi ya Edomu.+
7 Fahali mwitu watashuka pamoja nao,
Ng’ombe dume wachanga watashuka pamoja na wenye nguvu.
Nchi yao itajaa damu,
Na mavumbi yao yatalowa mafuta.”
8 Kwa maana Yehova ana siku ya kisasi,+
Mwaka wa malipo ya kesi dhidi ya Sayuni.+