-
Ezekieli 38:4-6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Nitakugeuza na kutia kulabu katika mataya yako+ na kukutoa pamoja na jeshi lako lote,+ farasi na wapanda farasi, wote wakiwa wamevaa mavazi ya kifahari, kusanyiko kubwa sana lenye ngao kubwa na ngao ndogo,* wote wakiwa na mapanga; 5 Uajemi, Ethiopia, na Putu+ wako pamoja nao, wote wakiwa na ngao ndogo na kofia; 6 Gomeri na wanajeshi wake wote, watu wa nyumba ya Togarma+ kutoka sehemu za mbali zaidi za kaskazini, pamoja na wanajeshi wake wote—mataifa mengi yako pamoja nawe.+
-
-
Ufunuo 19:17, 18Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Nikaona pia malaika amesimama katika jua, naye akaita kwa sauti kubwa na kuwaambia ndege wote wanaoruka katikati ya mbingu:* “Njooni hapa, mkusanyike pamoja kwenye mlo mkubwa wa jioni wa Mungu,+ 18 ili mle nyama za wafalme na nyama za viongozi wa kijeshi na nyama za watu wenye nguvu+ na nyama za farasi na za wale wanaoketi juu yao,+ na nyama za wote, za watu huru na vilevile za watumwa na za wadogo kwa wakubwa.”
-