-
Ezekieli 29:3, 4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Sema maneno haya: ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi:
“Niko dhidi yako, Farao mfalme wa Misri,+
Mnyama mkubwa sana wa baharini anayelala kati ya vijito vya mto wake Nile,*+
Ambaye amesema, ‘Mto wangu Nile ni wangu.
Niliutengeneza kwa ajili yangu.’+
4 Lakini nitatia kulabu katika mataya yako na kufanya samaki wa mto wako Nile washikamane na magamba yako.
Nitakutoa katika mto wako Nile pamoja na samaki wa mto wako Nile wanaoshikamana na magamba yako.
-