Ezekieli 47:3 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 3 Mtu huyo alipotoka nje kuelekea mashariki akiwa na kamba ya kupimia mkononi mwake,+ alipima mikono 1,000* na kunipitisha katika maji; maji hayo yalifika kwenye vifundo vya miguu. Zekaria 2:1, 2 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 2 Nami nikatazama juu na kumwona mtu akiwa na kamba ya kupimia+ mkononi mwake. 2 Kwa hiyo nikamuuliza: “Unaenda wapi?” Akanijibu: “Naenda kupima jiji la Yerusalemu, ili nijue upana wake na urefu wake.”+ Ufunuo 11:1 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 11 Nami nikapewa utete unaofanana na fimbo,*+ nikaambiwa: “Simama upime patakatifu pa hekalu la Mungu na madhabahu na wale wanaoabudu ndani yake. Ufunuo 21:15 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 15 Basi yule aliyekuwa akizungumza nami alikuwa ameshika utete wa kupimia wa dhahabu ili alipime lile jiji na malango yake na ukuta wake.+
3 Mtu huyo alipotoka nje kuelekea mashariki akiwa na kamba ya kupimia mkononi mwake,+ alipima mikono 1,000* na kunipitisha katika maji; maji hayo yalifika kwenye vifundo vya miguu.
2 Nami nikatazama juu na kumwona mtu akiwa na kamba ya kupimia+ mkononi mwake. 2 Kwa hiyo nikamuuliza: “Unaenda wapi?” Akanijibu: “Naenda kupima jiji la Yerusalemu, ili nijue upana wake na urefu wake.”+
11 Nami nikapewa utete unaofanana na fimbo,*+ nikaambiwa: “Simama upime patakatifu pa hekalu la Mungu na madhabahu na wale wanaoabudu ndani yake.
15 Basi yule aliyekuwa akizungumza nami alikuwa ameshika utete wa kupimia wa dhahabu ili alipime lile jiji na malango yake na ukuta wake.+