-
1 Mambo ya Nyakati 9:26, 27Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
26 Kulikuwa na walinzi wakuu* wanne waliowekwa katika wadhifa huo wa kuaminiwa. Walikuwa Walawi, nao walisimamia vyumba* na hazina za nyumba ya Mungu wa kweli.+ 27 Walikuwa wakikesha usiku kucha katika vituo vyao kuzunguka nyumba yote ya Mungu wa kweli, kwa maana walishughulikia utumishi wa ulinzi na kutunza ufunguo, nao walikuwa wakifungua nyumba hiyo asubuhi baada ya asubuhi.
-