-
Mambo ya Walawi 6:12, 13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Ni lazima moto wa madhabahu uendelee kuwaka. Haupaswi kuzimika. Kila asubuhi kuhani ataongeza kuni+ kwenye moto huo na kupanga dhabihu ya kuteketezwa juu yake, naye atateketeza mafuta ya dhabihu za ushirika ili yafuke moshi.+ 13 Hakikisheni kwamba moto unaendelea kuwaka daima kwenye madhabahu. Haupaswi kuzimika.
-
-
2 Mambo ya Nyakati 13:10, 11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 Lakini sisi, Yehova ndiye Mungu wetu,+ nasi hatujamwacha; makuhani wetu, wazao wa Haruni, wanamhudumia Yehova, na Walawi wanawasaidia kazi. 11 Wanamfukizia Yehova moshi wa dhabihu za kuteketezwa kila asubuhi na kila jioni+ pamoja na uvumba uliotiwa manukato,+ na mikate ya tabaka*+ iko kwenye meza iliyotengenezwa kwa dhahabu safi, nao wanawasha kinara cha taa cha dhahabu+ na taa zake kila jioni,+ kwa sababu tunatekeleza jukumu letu kwa Yehova Mungu wetu; lakini ninyi mmemwacha.
-