-
Yoshua 2:17-19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Wanaume hao wakasema: “Hatutakuwa na hatia kuhusiana na kiapo ulichotuapisha+ 18 isipokuwa, tutakapokuja katika nchi hii, utakuwa umefunga kamba hii nyekundu katika dirisha ambamo utatuteremshia. Wakusanye baba yako, mama yako, ndugu zako, na familia yote ya baba yako ndani ya nyumba hii.+ 19 Ikiwa mtu yeyote atatoka nje ya nyumba yako, damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe, nasi hatutakuwa na hatia. Lakini mtu yeyote aliye ndani ya nyumba yako pamoja nawe akifa, damu yake itakuwa juu ya vichwa vyetu.
-