-
Ezekieli 10:15-17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Na wale makerubi walikuwa wakiinuka—walikuwa viumbe hai walewale niliowaona* kwenye mto Kebari+— 16 na wale makerubi waliposonga, magurudumu yalikuwa yakisonga kando yao; na wale makerubi walipoinua juu mabawa yao ili yawe juu sana ya dunia, magurudumu hayo hayakuwa yakigeuka au kuondoka kando yao.+ 17 Waliposimama tuli, nayo yalisimama tuli; nao walipoinuka, yaliinuka pamoja nao, kwa maana roho iliyokuwa ikitenda katika wale viumbe hai* ilikuwa ndani ya magurudumu.
-