6 Kisha wakamkamata mfalme+ na kumpeleka mpaka kwa mfalme wa Babiloni kule Ribla, nao wakamhukumu. 7 Wakawachinja wana wa Sedekia huku akitazama; kisha Nebukadneza akampofusha macho Sedekia, akamfunga kwa pingu za shaba, na kumpeleka Babiloni.+
3 Nawe hutaponyoka kutoka mikononi mwake, kwa maana kwa hakika utakamatwa na kutiwa mikononi mwake.+ Nawe utamwona Mfalme wa Babiloni jicho kwa jicho, naye atazungumza nawe uso kwa uso, nawe utapelekwa Babiloni.’+
16 “‘“Kwa hakika kama ninavyoishi,” asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, “atafia huko Babiloni, mahali ambapo anaishi mfalme* aliyemweka* kuwa mfalme, ambaye alikidharau kiapo chake na ambaye alilivunja agano lake.+