-
Yeremia 32:4, 5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 na Mfalme Sedekia wa Yuda hataponyoka kutoka kwa Wakaldayo, kwa maana hakika atatiwa mikononi mwa mfalme wa Babiloni, naye atazungumza naye uso kwa uso na kumwona jicho kwa jicho.”+ 5 ‘Atampeleka Sedekia Babiloni, naye atakaa huko mpaka nitakapomkazia fikira,’ asema Yehova. ‘Ingawa mnaendelea kupigana na Wakaldayo, hamtafanikiwa.’”+
-
-
Ezekieli 12:12, 13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Mkuu aliye miongoni mwao atabeba mizigo yake begani na kuondoka kukiwa na giza. Atatoboa shimo ukutani na kuibeba mizigo yake kupitia humo.+ Ataufunika uso wake ili asione chini.’ 13 Nitautandaza wavu wangu juu yake, naye atakamatwa katika wavu wangu wa kuwindia.+ Kisha nitampeleka Babiloni, kwenye nchi ya Wakaldayo, lakini hataiona; naye atafia huko.+
-