3 Msifanye kama wanavyofanya katika nchi ya Misri ambako mliishi, wala msifanye kama wanavyofanya katika nchi ya Kanaani ambako nawapeleka.+ Msifuate sheria zao.
16 (Kwa maana ninyi mnajua vizuri jinsi tulivyoishi nchini Misri na jinsi tulivyopita katikati ya mataifa mbalimbali tulipokuwa safarini.+17 Nanyi mlikuwa mkiona vitu vyao vinavyochukiza na sanamu zao zenye kuchukiza*+ za miti na mawe, fedha na dhahabu, walizokuwa nazo.)
14 “Kwa hiyo, mwogopeni Yehova na kumtumikia kwa utimilifu* na uaminifu,*+ ondoeni miungu ambayo mababu zenu waliabudu ng’ambo ya Mto* na nchini Misri,+ nanyi mtumikieni Yehova.