-
Danieli 3:26, 27Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
26 Nebukadneza akaukaribia mlango wa lile tanuru lenye moto mkali na kusema: “Shadraki, Meshaki, na Abednego, ninyi watumishi wa Mungu Aliye Juu Zaidi,+ tokeni nje, mje hapa!” Shadraki, Meshaki, na Abednego wakatoka katikati ya moto. 27 Na maliwali, wasimamizi, magavana, na maofisa wakuu wa mfalme waliokuwa wamekusanyika mahali hapo+ wakaona kwamba moto haukuwadhuru* wanaume hao;+ hakuna unywele hata mmoja wa vichwa vyao uliokuwa umeungua, majoho yao hayakuwa yamebadilika, na miili yao haikuwa hata na harufu ya moto.
-