25 Atasema maneno dhidi ya Aliye Juu Zaidi,+ naye ataendelea kuwanyanyasa watakatifu wa Aliye Mkuu Zaidi. Atakusudia kubadili nyakati na sheria, nao watatiwa mikononi mwake kwa wakati, nyakati, na nusu wakati.*+
27 “‘Na ufalme na utawala na utukufu wa falme chini ya mbingu zote ulikabidhiwa watu ambao ni watakatifu wa Aliye Mkuu Zaidi.+ Ufalme wao ni ufalme wa milele,+ na tawala zote zitawatumikia na kuwatii wao.’