-
Danieli 12:7Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 Kisha nikamsikia yule mwanamume aliyevaa mavazi ya kitani, aliyekuwa juu ya maji ya kijito, alipokuwa akiinua mkono wake wa kulia na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni na kuapa hivi kwa jina la Yule anayeishi milele:+ “Itakuwa ni kwa wakati uliowekwa, nyakati zilizowekwa, na nusu ya wakati.* Mara tu kuvunjwavunjwa kwa nguvu za watu watakatifu kutakapofikia mwisho,+ mambo haya yote yatafikia mwisho wake.”
-
-
Ufunuo 13:5-7Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 Akapewa kinywa kinachosema mambo makuu na makufuru, akapewa pia mamlaka ya kutenda kwa miezi 42.+ 6 Naye akafungua kinywa chake kwa kumkufuru+ Mungu ili kulikufuru jina lake na makao yake, na hata wale wanaokaa mbinguni.+ 7 Akapewa ruhusa ya kupigana vita na watakatifu na kuwashinda,+ na akapewa mamlaka juu ya kila kabila na watu na lugha na taifa.
-