-
Danieli 2:40-42Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
40 “Ufalme wa nne utakuwa wenye nguvu kama chuma.+ Kwa maana kama vile chuma kinavyopondaponda na kusagasaga vitu vingine vyote, naam, kama chuma kinachovunjavunja, ufalme huo utapondaponda na kuzivunjavunja falme hizo zote.+
41 “Na kama tu ulivyoona kwamba nyayo na vidole vya miguu kwa sehemu vilikuwa vya udongo wa mfinyanzi na kwa sehemu vilikuwa vya chuma, ufalme huo utagawanyika, lakini ugumu fulani wa chuma utakuwa ndani yake, kama tu ulivyoona chuma kikiwa kimechanganyika na udongo laini wa mfinyanzi. 42 Na kama vile vidole vyake vya miguu vilikuwa kwa sehemu vya chuma na kwa sehemu vya udongo wa mfinyanzi, ndivyo ufalme huo utakavyokuwa na nguvu kwa sehemu na kuwa dhaifu kwa sehemu.
-