8 Hakutambua kwamba mimi ndiye niliyempa nafaka,+ divai mpya, na mafuta,
Na mimi ndiye niliyempa fedha nyingi
Na dhahabu, waliyotumia kumtumikia Baali.+
9 ‘Kwa hiyo, nitarudi na kuchukua nafaka yangu itakapokomaa
Na divai yangu mpya katika majira yake,+
Nami nitampokonya sufu yangu na kitani changu kilichokusudiwa kufunika uchi wake.