4 Sikieni hili, ninyi mnaowakandamiza maskini
Na kuwaangamiza wapole nchini,+
5 Mnaosema, ‘Sherehe ya mwezi mpya itakwisha lini,+ ili tuuze nafaka yetu,
Na Sabato+ itakwisha lini, tukauze nafaka?
Ili tupunguze kipimo cha efa
Na kuongeza uzito wa shekeli,
Kuipotosha mizani yetu ya udanganyifu;+
6 Ili tuwanunue wenye uhitaji kwa fedha
Na maskini kwa jozi ya viatu,+
Na kuuza makapi ya nafaka.’