14 Mtakusanyika asubuhi, kabila kwa kabila, na kabila ambalo Yehova atachagua+ litakaribia, ukoo kwa ukoo, na ukoo ambao Yehova atachagua utakaribia, nyumba kwa nyumba, na nyumba ambayo Yehova atachagua itakaribia, mwanamume kwa mwanamume.
18 Mwishowe akaleta karibu familia ya Zabdi, mwanamume kwa mwanamume, naye Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, wa kabila la Yuda, akachaguliwa.+
42 Basi Sauli akasema: “Pigeni kura+ kuamua kati yangu na mwanangu Yonathani.” Kisha Yonathani akachaguliwa. 43 Halafu Sauli akamuuliza Yonathani: “Niambie, umefanya nini?” Yonathani akamwambia: “Nilionja tu asali kidogo kwa ncha ya fimbo iliyo mikononi mwangu.+ Nipo hapa! Niko tayari kufa!”