-
Yeremia 39:5-7Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 Lakini jeshi la Wakaldayo likawafuatia, nao wakamfikia Sedekia katika jangwa tambarare la Yeriko.+ Wakamkamata na kumleta kwa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni kule Ribla+ katika nchi ya Hamathi,+ ambako alimhukumu. 6 Mfalme wa Babiloni akaagiza wana wa Sedekia wachinjwe mbele ya macho yake kule Ribla, na mfalme wa Babiloni akaagiza wakuu wote wa Yuda wachinjwe.+ 7 Ndipo akayapofusha macho ya Sedekia, kisha akamfunga kwa pingu za shaba ili ampeleke Babiloni.+
-
-
Danieli 5:18, 19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 Ee mfalme, Mungu Aliye Juu Zaidi alimpa baba yako Nebukadneza ufalme na ukuu na heshima na fahari.+ 19 Kwa sababu ya ukuu ambao Mungu alimpa, watu wa makabila yote, mataifa, na lugha walitetemeka kwa woga mbele yake.+ Yeyote ambaye mfalme alitaka kumuua, alimuua, yeyote aliyetaka kumwacha hai, alimwacha hai, yeyote aliyetaka kumkweza, alimkweza, na yeyote aliyetaka kumwaibisha, alimwaibisha.+
-