-
2 Wafalme 25:8-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Katika mwezi wa tano, siku ya saba ya mwezi huo, yaani, mwaka wa 19 wa utawala wa Mfalme Nebukadneza wa Babiloni, Nebuzaradani+ mkuu wa walinzi, mtumishi wa mfalme wa Babiloni, alikuja Yerusalemu.+ 9 Akateketeza kabisa nyumba ya Yehova,+ nyumba ya mfalme,*+ na nyumba zote Yerusalemu;+ aliteketeza pia nyumba ya kila mtu maarufu.+ 10 Na jeshi lote la Wakaldayo lililokuwa pamoja na mkuu wa walinzi lilibomoa kuta zilizozunguka Yerusalemu.+
-
-
Yeremia 52:12-14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Katika mwezi wa tano, siku ya kumi ya mwezi huo, yaani, mwaka wa 19 wa utawala wa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni, Nebuzaradani mkuu wa walinzi, aliyekuwa mhudumu wa mfalme wa Babiloni, aliingia Yerusalemu.+ 13 Akateketeza kabisa nyumba ya Yehova,+ nyumba ya* mfalme, na nyumba zote za Yerusalemu; aliteketeza pia kila nyumba kubwa. 14 Na jeshi lote la Wakaldayo lililokuwa pamoja na mkuu wa walinzi lilibomoa kuta zilizozunguka Yerusalemu.+
-