Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 9:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Na nyumba hii itakuwa marundo ya magofu.+ Kila mtu atakayepita karibu nayo ataitazama kwa mshangao, atapiga mluzi na kuuliza, ‘Kwa nini Yehova aliitendea hivi nchi hii na nyumba hii?’+

  • 2 Mambo ya Nyakati 36:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Kwa hiyo akamleta mfalme wa Wakaldayo awashambulie,+ ambaye aliwaua wanaume wao vijana kwa upanga+ katika nyumba ya mahali pao patakatifu;+ hakumhurumia kijana wa kiume wala bikira, mzee wala aliye dhaifu.+ Mungu alitia kila kitu mikononi mwake.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 36:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Aliiteketeza kabisa nyumba ya Mungu wa kweli,+ akaubomoa ukuta wa Yerusalemu,+ akateketeza kwa moto minara yake yote yenye ngome, na kuharibu kila kitu chenye thamani.+

  • Zaburi 74:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  8 Wao pamoja na uzao wao wamesema mioyoni mwao:

      “Sehemu zote za Mungu za mikutano* zilizo nchini ni lazima ziteketezwe.”

  • Zaburi 79:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 79 Ee Mungu, mataifa yamevamia urithi wako;+

      Yamelichafua hekalu lako takatifu;+

      Yamebadili Yerusalemu kuwa rundo la magofu.+

  • Yeremia 26:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 “Mika+ wa Moreshethi alikuwa akitabiri katika siku za utawala wa Mfalme Hezekia+ wa Yuda, akawaambia watu wote wa Yuda, ‘Yehova wa majeshi anasema hivi:

      “Sayuni litalimwa kama shamba,

      Yerusalemu litakuwa marundo ya magofu,+

      Na mlima wa Nyumba* utakuwa kama vilima msituni.”’*+

  • Maombolezo 2:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Yehova ameikataa madhabahu yake;

      Amedharau mahali pake patakatifu.+

      Amesalimisha kuta za minara yake yenye ngome mikononi mwa adui.+

      Wameinua sauti yao ndani ya nyumba ya Yehova,+ kama inavyokuwa siku ya sherehe.

  • Ezekieli 24:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 ‘Waambie watu wa nyumba ya Israeli, “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Niko karibu kupatia unajisi mahali pangu patakatifu,+ chanzo cha fahari yenu kubwa, kitu mnachokipenda sana na tamaa ya moyo wenu.* Wana na mabinti wenu mliowaacha watauawa kwa upanga.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki