-
2 Mambo ya Nyakati 36:17-19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Kwa hiyo akamleta mfalme wa Wakaldayo awashambulie,+ ambaye aliwaua wanaume wao vijana kwa upanga+ katika nyumba ya mahali pao patakatifu;+ hakumhurumia kijana wa kiume wala bikira, mzee wala aliye dhaifu.+ Mungu alitia kila kitu mikononi mwake.+ 18 Alipeleka kila kitu Babiloni, vyombo vyote vya nyumba ya Mungu wa kweli, vikubwa na vidogo, na pia hazina za nyumba ya Yehova na hazina za mfalme na wakuu wake.+ 19 Aliiteketeza kabisa nyumba ya Mungu wa kweli,+ akaubomoa ukuta wa Yerusalemu,+ akateketeza kwa moto minara yake yote yenye ngome, na kuharibu kila kitu chenye thamani.+
-