Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 20:16, 17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Sasa Isaya akamwambia Hezekia: “Sikia neno la Yehova,+ 17 ‘Tazama! Siku zinakuja, na vitu vyote vilivyo katika nyumba yako* na vitu vyote ambavyo mababu zako wamehifadhi mpaka leo hii vitapelekwa Babiloni.+ Hakuna chochote kitakachobaki,” asema Yehova.

  • Isaya 39:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 ‘Tazama! Siku zinakuja, na vitu vyote vilivyo katika nyumba yako* na vitu vyote ambavyo mababu zako wamehifadhi mpaka leo hii vitapelekwa Babiloni. Hakuna chochote kitakachobaki,’+ asema Yehova.+

  • Yeremia 27:19-22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 “Kwa maana Yehova wa majeshi anasema hivi kuhusu zile nguzo,+ ile Bahari,*+ yale magari,+ na vyombo vilivyobaki vilivyoachwa katika jiji hili, 20 ambavyo Mfalme Nebukadneza wa Babiloni hakuvichukua alipompeleka uhamishoni Yekonia mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, kutoka Yerusalemu hadi Babiloni, pamoja na watu wote wenye vyeo wa Yuda na Yerusalemu;+ 21 naam, Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi kuhusu vyombo vilivyobaki katika nyumba ya Yehova, katika nyumba ya* mfalme wa Yuda, na Yerusalemu: 22 ‘“Vitapelekwa Babiloni,+ navyo vitabaki huko mpaka siku nitakapovikazia fikira,” asema Yehova. “Kisha nitavileta na kuvirudisha mahali hapa.”’”+

  • Yeremia 52:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Pia Wakaldayo walivunja vipandevipande nguzo za shaba+ za nyumba ya Yehova na magari+ na Bahari ya shaba,+ vitu vilivyokuwa katika nyumba ya Yehova, nao wakaipeleka shaba yote hiyo Babiloni.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki