-
Yeremia 27:19-22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
19 “Kwa maana Yehova wa majeshi anasema hivi kuhusu zile nguzo,+ ile Bahari,*+ yale magari,+ na vyombo vilivyobaki vilivyoachwa katika jiji hili, 20 ambavyo Mfalme Nebukadneza wa Babiloni hakuvichukua alipompeleka uhamishoni Yekonia mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, kutoka Yerusalemu hadi Babiloni, pamoja na watu wote wenye vyeo wa Yuda na Yerusalemu;+ 21 naam, Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi kuhusu vyombo vilivyobaki katika nyumba ya Yehova, katika nyumba ya* mfalme wa Yuda, na Yerusalemu: 22 ‘“Vitapelekwa Babiloni,+ navyo vitabaki huko mpaka siku nitakapovikazia fikira,” asema Yehova. “Kisha nitavileta na kuvirudisha mahali hapa.”’”+
-