Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 24:14, 15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Akawapeleka uhamishoni watu wote wa Yerusalemu, wakuu wote,+ mashujaa wote hodari, na kila fundi na mfua chuma*+—aliwapeleka uhamishoni watu 10,000. Hakuna yeyote aliyebaki isipokuwa watu maskini kabisa nchini.+ 15 Basi akampeleka Yehoyakini+ uhamishoni Babiloni;+ alimpeleka pia mama ya mfalme, wake za mfalme, maofisa wa makao yake, na viongozi wa nchi, akawapeleka uhamishoni Babiloni kutoka Yerusalemu.

  • 2 Mambo ya Nyakati 36:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Mwanzoni mwa mwaka,* Mfalme Nebukadneza aliagiza aletwe Babiloni,+ pamoja na vyombo vyenye thamani vya nyumba ya Yehova.+ Akamweka Sedekia ndugu ya baba yake kuwa mfalme wa Yuda na Yerusalemu.+

  • Yeremia 24:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Kisha Yehova akanionyesha vikapu viwili vya tini vilivyowekwa mbele ya hekalu la Yehova, baada ya Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni kumpeleka uhamishoni Yekonia*+ mwana wa Yehoyakimu,+ mfalme wa Yuda, pamoja na wakuu wa Yuda, mafundi, na wahunzi;* aliwatoa Yerusalemu na kuwapeleka Babiloni.+

  • Danieli 1:2, 3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Baada ya muda Yehova akamtia Mfalme Yehoyakimu wa Yuda mikononi mwake,+ pamoja na baadhi ya vyombo vya nyumba ya* Mungu wa kweli, akavileta katika nchi ya Shinari*+ katika nyumba ya* mungu wake. Akaviweka katika hazina ya mungu wake.+

      3 Kisha Mfalme Nebukadneza akamwagiza Ashpenazi ofisa mkuu wa makao yake ya kifalme awalete baadhi ya Waisraeli,* kutia ndani wale wanaotoka katika uzao wa kifalme na wa watu mashuhuri.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki