Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 7:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Alitengeneza nguzo mbili kwa kutumia shaba iliyoyeyushwa;+ kila nguzo ilikuwa na urefu wa mikono 18, na kila moja ya nguzo hizo mbili ingeweza kuzungukwa kwa kamba yenye urefu wa mikono 12.*+

  • 2 Wafalme 25:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Kila nguzo ilikuwa na urefu wa mikono 18,*+ na kifuniko chake kilikuwa cha shaba; na urefu wa kifuniko hicho ulikuwa mikono mitatu, na wavu pamoja na makomamanga yote yaliyozunguka kifuniko yalitengenezwa kwa shaba.+ Nguzo ya pili pamoja na wavu wake ilifanana na ya kwanza.

  • 2 Mambo ya Nyakati 4:11, 12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Hiramu alitengeneza pia ndoo za kuondolea majivu, pia sepetu, na mabakuli.+

      Basi Hiramu akamaliza kazi yote aliyomfanyia Mfalme Sulemani kuhusiana na nyumba ya Mungu wa kweli:+ 12 zile nguzo mbili+ na vifuniko vyenye umbo la bakuli vilivyokuwa juu ya nguzo hizo; na nyavu mbili+ za kufunika vifuniko hivyo viwili vyenye umbo la bakuli vilivyokuwa juu ya nguzo hizo;

  • Yeremia 52:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Kuhusu nguzo, kila nguzo ilikuwa na kimo cha mikono 18,* na kamba ya kupimia yenye urefu wa mikono 12 ingeweza kuizunguka;+ unene wake ulikuwa upana wa vidole vinne,* na ndani ilikuwa wazi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki