-
2 Wafalme 24:12, 13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Mfalme Yehoyakini wa Yuda akatoka nje kwenda kukutana na mfalme wa Babiloni,+ akiwa pamoja na mama yake, watumishi wake, wakuu wake, na maofisa wa makao yake;+ na mfalme wa Babiloni akamchukua mateka katika mwaka wa nane wa utawala wake.+ 13 Kisha akachukua hazina zote za nyumba ya Yehova na hazina za nyumba ya mfalme.*+ Alivikata vipandevipande vyombo vyote vya dhahabu ambavyo Sulemani mfalme wa Israeli alitengeneza katika hekalu la Yehova.+ Hilo lilitendeka kama Yehova alivyokuwa ametabiri.
-
-
Yeremia 27:21, 22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
21 naam, Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi kuhusu vyombo vilivyobaki katika nyumba ya Yehova, katika nyumba ya* mfalme wa Yuda, na Yerusalemu: 22 ‘“Vitapelekwa Babiloni,+ navyo vitabaki huko mpaka siku nitakapovikazia fikira,” asema Yehova. “Kisha nitavileta na kuvirudisha mahali hapa.”’”+
-