-
Yeremia 52:17-20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Pia Wakaldayo walivunja vipandevipande nguzo za shaba+ za nyumba ya Yehova na magari+ na Bahari ya shaba,+ vitu vilivyokuwa katika nyumba ya Yehova, nao wakaipeleka shaba yote hiyo Babiloni.+ 18 Walichukua pia ndoo za kuondolea majivu, sepetu, mikasi ya kukatia tambi za taa, mabakuli,+ vikombe,+ na vyombo vyote vya shaba vilivyotumiwa katika utumishi wa hekaluni. 19 Mkuu wa walinzi alichukua mabeseni,+ vyetezo, mabakuli, ndoo za kuondolea majivu, vinara vya taa,+ vikombe, na mabakuli yaliyotengenezwa kwa dhahabu na fedha halisi.+ 20 Shaba yote iliyotumiwa kutengeneza zile nguzo mbili, wale ng’ombe dume 12 wa shaba+ waliokuwa chini ya ile Bahari, na yale magari ambayo Mfalme Sulemani alitengeneza kwa ajili ya nyumba ya Yehova, haingeweza kupimwa uzito.
-