-
2 Wafalme 25:13-16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Pia Wakaldayo walivunja vipandevipande nguzo za shaba+ za nyumba ya Yehova na magari+ na Bahari ya shaba,+ vitu vilivyokuwa katika nyumba ya Yehova, nao wakaipeleka shaba hiyo Babiloni.+ 14 Walichukua pia ndoo za kuondolea majivu, sepetu, mikasi ya kukatia tambi za taa, vikombe, na vyombo vyote vya shaba vilivyotumiwa katika utumishi wa hekaluni. 15 Mkuu wa walinzi alichukua vyetezo na mabakuli yaliyotengenezwa kwa dhahabu+ na fedha halisi.+ 16 Shaba yote iliyotumiwa kutengeneza zile nguzo mbili, ile Bahari, na yale magari ambayo Sulemani alitengeneza kwa ajili ya nyumba ya Yehova, haingeweza kupimwa uzito.+
-