-
Marko 1:40-44Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
40 Mtu fulani mwenye ukoma akamjia, akapiga magoti na kumwomba: “Ikiwa tu unataka, unaweza kunitakasa.”+ 41 Ndipo akamsikitikia, akanyoosha mkono wake, akamgusa na kumwambia: “Ninataka! Takasika.”+ 42 Mara moja ule ukoma ukaisha, akawa safi. 43 Kisha akampa maagizo thabiti na mara moja akamwacha aende, 44 akamwambia: “Usimwambie jambo lolote mtu yeyote, bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani na utoe vitu alivyoagiza Musa kwa ajili ya kutakaswa kwako,+ ili kuwa ushahidi kwao.”+
-
-
Luka 5:12-14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Pindi nyingine alipokuwa katika jiji fulani, tazama! kulikuwa na mwanamume aliyejaa ukoma! Alipomwona Yesu, akajiangusha kifudifudi na kumwomba: “Bwana, ikiwa tu unataka, unaweza kunitakasa.”+ 13 Basi Yesu akanyoosha mkono wake akamgusa na kusema: “Ninataka! Takasika.” Mara moja ule ukoma ukaisha.+ 14 Kisha akamwagiza mtu huyo asimwambie mtu yeyote: “Bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, kisha utoe toleo la kutakaswa kwako, kama alivyoagiza Musa,+ ili kuwa ushahidi kwao.”+
-