-
Marko 2:21, 22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
21 Hakuna mtu anayeshona kiraka cha kitambaa kipya juu ya vazi la nje la zamani. Akifanya hivyo, kitambaa kipya kitatoka kwenye vazi la zamani, nalo litararuka vibaya zaidi.+ 22 Pia, hakuna mtu anayeweka divai mpya katika viriba vya divai vilivyochakaa. Akifanya hivyo, divai itapasua ngozi ya viriba naye atapoteza divai pamoja na ngozi. Lakini divai mpya huwekwa katika viriba vipya vya divai.”
-
-
Luka 5:36-39Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
36 Pia, akawapa mfano: “Hakuna mtu anayekata kiraka cha vazi jipya la nje na kukishona kwenye vazi la zamani. Akifanya hivyo, kiraka kipya hurarua vazi la zamani na kiraka kipya hakilingani na vazi la zamani.+ 37 Pia, hakuna mtu anayeweka divai mpya katika viriba vya divai vilivyochakaa. Akifanya hivyo, divai mpya itavipasua viriba, nayo itamwagika na viriba vitaharibika. 38 Lakini divai mpya lazima iwekwe katika viriba vipya vya divai. 39 Mtu anapokunywa divai ya zamani hapendi divai mpya, kwa maana husema, ‘Ile ya zamani ndiyo nzuri.’”
-