Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 4:42-44
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 42 Mtu fulani alikuja kutoka Baal-shalisha,+ akamletea mtu wa Mungu wa kweli mikate 20 ya shayiri+ iliyookwa kwa shayiri iliyokomaa kwanza, pamoja na mfuko wa nafaka iliyotoka kuvunwa.+ Kisha Elisha akasema: “Wape watu ili wale.” 43 Hata hivyo, mtumishi wake akamuuliza: “Nitawezaje kuwapa wanaume 100 chakula hiki?”+ Elisha akasema: “Wape watu ili wale, kwa maana Yehova anasema hivi: ‘Watakula na kingine kitabaki.’”+ 44 Basi akawapa, nao wakala na kingine kikabaki,+ kama Yehova alivyosema.

  • Marko 6:42, 43
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 42 Basi wote wakala wakashiba, 43 nao wakakusanya vipande vilivyobaki na kujaza vikapu 12, bila kuhesabu samaki.+

  • Marko 8:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Basi wakala wakashiba, kisha wakakusanya vipande vilivyobaki wakajaza vikapu saba vikubwa.+

  • Luka 9:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Basi wote wakala wakashiba, nao wakakusanya chakula kilichobaki na kujaza vikapu 12.+

  • Yohana 6:12, 13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Waliposhiba akawaambia wanafunzi wake: “Kusanyeni vipande vilivyobaki, ili chochote kisipotee.” 13 Basi wakakusanya vipande vilivyobaki wakajaza vikapu 12 baada ya watu kula kutokana na ile mikate mitano ya shayiri.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki