-
Marko 9:43-48Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
43 “Ikiwa mkono wako unakufanya ukwazike, ukate. Ni afadhali uingie katika uzima ukiwa kilema kuliko kuingia ukiwa na mikono miwili katika Gehena,* katika moto usioweza kuzimwa.+ 44* —— 45 Na ikiwa mguu wako unakufanya ukwazike, ukate. Ni afadhali uingie katika uzima ukiwa kilema kuliko kutupwa katika Gehena* ukiwa na miguu miwili.+ 46* —— 47 Na ikiwa jicho lako linakufanya ukwazike, litupe mbali.+ Ni afadhali uingie katika Ufalme wa Mungu ukiwa na jicho moja kuliko kutupwa katika Gehena ukiwa na macho mawili,*+ 48 mahali ambapo funza hawafi na moto hauzimwi.+
-