-
Marko 10:13-16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Watu wakaanza kumletea watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wakawakemea.+ 14 Alipoona hivyo, Yesu akakasirika na kuwaambia: “Waacheni watoto wadogo waje kwangu; msijaribu kuwazuia, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama hao.+ 15 Kwa kweli ninawaambia, yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hataingia kamwe ndani yake.”+ 16 Akawachukua watoto akawakumbatia na kuanza kuwabariki, akiweka mikono yake juu yao.+
-
-
Luka 18:15-17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Sasa watu wakamletea Yesu watoto wao wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi walipoona hivyo wakaanza kuwakemea.+ 16 Lakini Yesu akawaita wale watoto, akisema: “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, na msijaribu kuwazuia, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama wao.+ 17 Kwa kweli ninawaambia, yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hataingia kamwe ndani yake.”+
-