-
Mathayo 19:13-15Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Ndipo watu wakamletea watoto wadogo ili aweke mikono yake juu yao na kusali, lakini wanafunzi wakawakemea.+ 14 Hata hivyo, Yesu akawaambia: “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, na msijaribu kuwazuia, kwa maana Ufalme wa mbinguni ni wa wale walio kama wao.”+ 15 Naye akaweka mikono yake juu yao kisha akaondoka hapo.
-
-
Marko 10:13-16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Watu wakaanza kumletea watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wakawakemea.+ 14 Alipoona hivyo, Yesu akakasirika na kuwaambia: “Waacheni watoto wadogo waje kwangu; msijaribu kuwazuia, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama hao.+ 15 Kwa kweli ninawaambia, yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hataingia kamwe ndani yake.”+ 16 Akawachukua watoto akawakumbatia na kuanza kuwabariki, akiweka mikono yake juu yao.+
-