-
Luka 10:25-28Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
25 Tazama! mtu fulani mwenye ujuzi wa Sheria akasimama ili amjaribu, akamuuliza: “Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?”+ 26 Yesu akamuuliza: “Ni mambo gani yameandikwa katika Sheria? Wewe unasomaje?” 27 Akajibu: “‘Lazima umpende Yehova* Mungu wako kwa moyo wako wote kwa nafsi* yako yote kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote’+ na ‘umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.’”+ 28 Akamwambia: “Umejibu vizuri; endelea kufanya hivyo nawe utapata uzima.”+
-