-
Marko 10:41-45Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
41 Wale wengine kumi waliposikia jambo hilo, wakawakasirikia Yakobo na Yohana.+ 42 Lakini Yesu akawaita akawaambia: “Mnajua kwamba wale wanaotawala* mataifa hupiga ubwana juu yao na wakuu wao hutumia mamlaka juu yao.+ 43 Haipaswi kuwa hivyo kati yenu; lakini yeyote anayetaka kuwa mkubwa kati yenu lazima awe mhudumu wenu,+ 44 na yeyote anayetaka kuwa wa kwanza kati yenu lazima awe mtumwa wa wote. 45 Kwa maana hata Mwana wa binadamu alikuja, si kuhudumiwa, bali kuhudumu+ na kutoa uhai wake uwe* fidia badala ya wengi.”+
-