-
Luka 19:32-35Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
32 Basi wale waliotumwa wakaenda na kupata sawasawa na vile Yesu alivyowaambia.+ 33 Lakini walipokuwa wakimfungua mwanapunda huyo, wenyewe wakawauliza: “Mbona mnamfungua huyo mwanapunda?” 34 Wakajibu: “Bwana anamhitaji.” 35 Wakampeleka kwa Yesu, nao wakaweka mavazi yao ya nje juu ya huyo mwanapunda na kumketisha Yesu juu yake.+
-