-
Marko 11:7-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 Wakampelekea Yesu huyo mwanapunda,+ wakatandika mavazi yao ya nje juu yake, naye akaketi juu yake.+ 8 Pia, wengi wakatandaza mavazi yao ya nje barabarani, lakini wengine wakatandaza matawi ya miti waliyokata katika mashamba.+ 9 Watu waliokuwa mbele na wale waliofuata nyuma wakaendelea kupaza sauti: “Tunaomba umwokoe!+ Amebarikiwa yule anayekuja katika jina la Yehova!*+ 10 Umebarikiwa Ufalme unaokuja wa baba yetu Daudi!+ Tunaomba umwokoe, katika vilele vilivyo juu!”
-