Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 38:7, 8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Lakini Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alimchukiza Yehova; kwa hiyo Yehova akamuua. 8 Kwa hiyo, Yuda akamwambia Onani: “Lala na mke wa ndugu yako na ufunge naye ndoa ya ndugu mkwe, umpe ndugu yako mzao.”+

  • Kumbukumbu la Torati 25:5, 6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 “Ikiwa ndugu wanaishi pamoja na mmoja wao afe bila mwana, mke wa yule aliyekufa hapaswi kuolewa na mwanamume mwingine nje ya ukoo huo. Ndugu ya mume wake anapaswa kwenda kwake, amchukue awe mke wake, na kufunga naye ndoa ya ndugu mkwe.+ 6 Mtoto wa kwanza atakayemzaa ataendeleza jina la ndugu yake aliyekufa,+ ili jina lake lisifutiliwe mbali kutoka Israeli.+

  • Ruthu 1:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Lakini Naomi akawaambia: “Rudini binti zangu. Kwa nini mnifuate? Je, ninaweza tena kuzaa watoto ambao watakuwa waume zenu?+

  • Ruthu 3:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Kaa hapa usiku wa leo, na ikiwa atakukomboa asubuhi, ni sawa! Na akukomboe.+ Lakini ikiwa hataki kukukomboa, kwa hakika kama Yehova anavyoishi, mimi mwenyewe nitakukomboa. Lala hapa mpaka asubuhi.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki