-
Marko 12:24-27Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 Yesu akawaambia: “Ninyi mmekosea kwa sababu hamjui Maandiko wala nguvu za Mungu.+ 25 Kwa maana wanapofufuliwa kutoka kwa wafu, wanaume hawaoi wala wanawake hawaolewi, bali wao ni kama malaika mbinguni.+ 26 Lakini kuhusu kufufuliwa kwa wafu, je, hamkusoma katika kitabu cha Musa, simulizi kuhusu kile kichaka cha miiba kwamba Mungu alimwambia: ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo’?+ 27 Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai. Mmekosea sana.”+
-