-
Luka 20:34-36Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
34 Yesu akawaambia: “Watoto wa mfumo huu wa mambo* huoa na kuolewa, 35 lakini wale waliohesabiwa kuwa wanastahili kuupata mfumo huo wa mambo na kufufuliwa kutoka kwa wafu hawaoi wala kuolewa.+ 36 Kwa kweli, hawawezi kufa tena kamwe, kwa maana wao ni kama malaika, nao ni watoto wa Mungu kwa kuwa watoto wa ufufuo.
-