-
2 Mambo ya Nyakati 24:20-22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
20 Roho ya Mungu ikamjia* Zekaria mwana wa kuhani Yehoyada,+ naye akasimama mahali palipo juu mbele ya watu na kuwaambia: “Mungu wa kweli anasema hivi: ‘Kwa nini mnazivunja amri za Yehova? Hamtafanikiwa! Kwa sababu mmemwacha Yehova, yeye naye, atawaacha ninyi.’”+ 21 Lakini walipanga njama dhidi yake,+ wakampiga mawe katika ua wa nyumba ya Yehova, kwa agizo la mfalme.+ 22 Kwa hiyo Mfalme Yehoashi hakukumbuka upendo mshikamanifu ambao Yehoyada baba yake* alimtendea, alimuua mwanawe, ambaye alisema hivi alipokuwa akifa: “Yehova na ashughulikie jambo hili na kukulipiza kisasi.”+
-