25 “Pia, kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota,+ na duniani mataifa yatakuwa na maumivu makali bila kujua cha kufanya kwa sababu ya mngurumo na msukosuko wa bahari. 26 Watu watazimia kwa woga wakitarajia mambo yatakayotokea juu ya dunia inayokaliwa, kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.