-
Marko 15:6-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Basi, kila sherehe ya Pasaka, alikuwa na desturi ya kuwafungulia mfungwa ambaye waliomba.+ 7 Wakati huo mtu aliyeitwa Baraba alikuwa amefungwa pamoja na wachochezi ambao katika uchochezi wao walikuwa wameua. 8 Basi umati ukaja na kuanza kumwomba Pilato awafanyie kama ilivyokuwa desturi yake. 9 Akawauliza: “Je, mnataka niwafungulie Mfalme wa Wayahudi?”+ 10 Kwa maana Pilato alijua kwamba wakuu wa makuhani walikuwa wamemkabidhi Yesu kwake kwa sababu ya wivu.+
-