-
Luka 23:50-53Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
50 Na tazama! kulikuwa na mwanamume aliyeitwa Yosefu, mshiriki wa Baraza, ambaye alikuwa mtu mwema na mwadilifu.+ 51 (Mtu huyo hakupiga kura kuunga mkono njama na kitendo chao.) Alikuwa wa kutoka Arimathea, jiji la Wayudea, naye alikuwa akiungojea Ufalme wa Mungu. 52 Mtu huyo alienda kwa Pilato akaomba apewe mwili wa Yesu. 53 Naye akaushusha+ na kuufunga kwa kitani bora, akaulaza katika kaburi* lililochongwa kwenye mwamba,+ ambamo hakuna mtu aliyewahi kulazwa.
-