-
Kumbukumbu la Torati 21:22, 23Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
22 “Mtu akitenda dhambi inayostahili hukumu ya kifo, naye ameuawa,+ na mmemtundika mtini,+ 23 maiti yake isibaki mtini usiku kucha.+ Badala yake, mnapaswa kuhakikisha kwamba mnaizika siku hiyohiyo, kwa sababu mtu aliyetundikwa ni kitu kilicholaaniwa na Mungu,+ nanyi hampaswi kuichafua nchi ambayo Yehova Mungu wenu anawapa iwe urithi wenu.+
-
-
Luka 23:50-52Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
50 Na tazama! kulikuwa na mwanamume aliyeitwa Yosefu, mshiriki wa Baraza, ambaye alikuwa mtu mwema na mwadilifu.+ 51 (Mtu huyo hakupiga kura kuunga mkono njama na kitendo chao.) Alikuwa wa kutoka Arimathea, jiji la Wayudea, naye alikuwa akiungojea Ufalme wa Mungu. 52 Mtu huyo alienda kwa Pilato akaomba apewe mwili wa Yesu.
-