Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 21:22, 23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 “Mtu akitenda dhambi inayostahili hukumu ya kifo, naye ameuawa,+ na mmemtundika mtini,+ 23 maiti yake isibaki mtini usiku kucha.+ Badala yake, mnapaswa kuhakikisha kwamba mnaizika siku hiyohiyo, kwa sababu mtu aliyetundikwa ni kitu kilicholaaniwa na Mungu,+ nanyi hampaswi kuichafua nchi ambayo Yehova Mungu wenu anawapa iwe urithi wenu.+

  • Mathayo 27:57, 58
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 57 Sasa kwa kuwa ilikuwa jioni, akaja tajiri mmoja wa Arimathea, aitwaye Yosefu, ambaye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.+ 58 Mtu huyu alienda kwa Pilato akaomba apewe mwili wa Yesu.+ Naye Pilato akaamuru apewe.+

  • Luka 23:50-52
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 50 Na tazama! kulikuwa na mwanamume aliyeitwa Yosefu, mshiriki wa Baraza, ambaye alikuwa mtu mwema na mwadilifu.+ 51 (Mtu huyo hakupiga kura kuunga mkono njama na kitendo chao.) Alikuwa wa kutoka Arimathea, jiji la Wayudea, naye alikuwa akiungojea Ufalme wa Mungu. 52 Mtu huyo alienda kwa Pilato akaomba apewe mwili wa Yesu.

  • Yohana 19:38
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 38 Baada ya mambo hayo Yosefu wa Arimathea, aliyekuwa mwanafunzi wa Yesu lakini kwa siri kwa sababu aliwaogopa Wayahudi,+ akamwomba ruhusa Pilato ili auondoe mwili wa Yesu, naye Pilato akamruhusu. Basi akaja na kuuondoa mwili huo.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki