-
Mathayo 15:15-20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Petro akamwambia: “Tufafanulie mfano huo.” 16 Ndipo akasema: “Je, ninyi pia bado hamwelewi?+ 17 Je, hamjui kwamba chochote kinachoingia kinywani hupita tumboni kisha hutoka na kuingia chooni? 18 Hata hivyo, mambo yanayotoka kinywani hutoka moyoni, nayo ndiyo yanayomchafua mtu.+ 19 Kwa mfano, moyoni hutoka mawazo mabaya,+ mauaji, uzinzi, uasherati,* wizi, ushahidi wa uwongo, na makufuru. 20 Hayo ndiyo mambo yanayomchafua mtu; lakini kula bila kunawa* mikono hakumchafui mtu.”
-